Sunday 15 January 2017

UZINDUZI WA MAZOEZI KWA MATUMISHI WA UMMA KATIKA HALMASHAURI YA BUHIGWE



"Mazoezi ni afya"
 Kupitia ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe mkoa Kigoma, siku ya Jumamosi (14.01.2017) ilizindua rasmi mazoezi kwa watumishi wa Halmashauri. "Lengo kuu ya mazoezi hayo nijenga mwili na kujiepusha na magonjwa yasio ambukiza, kama vile ugonjwa wa presha ya damu, kuongezeka uzito niongoni mwatatizo kubwa kwa wengi mwa watumishi wa umma, kupitia mazoezi hayo ambayo yanataraji kufanyika kila jumamosi ya wiki ya pili ya mwezi"

Mkuu wa wilaya akataja faida zipatikanazo kwa kufanya mazoezi.
1. Mazoezi ya mwili husaidia kulirekebisha shinikizo la Damu.
2.  Mazoezi ya Mwili huiruhusu damu nyingi zaidi kuzifikia sehemu zote za mwili na kuifanya mikono na miguu ipate joto.
3. Mazoezi ya mwili yanaondoa mambo yote ya mwili, yaani mkazo wa mwili na mfashaiko wa moyo na kukusaidia wewe kujisikia vizuri zaidi katika maisha yako. Mazoezi ni tiba bora.
4. Mazoezi ya mwili hujenga afya yako
5. Mazoezi ya mwili huimarisha misuli pia nakunawirisha mwili kwa ujumla
6. Mazoezi huongeza ufanisi makazini

Mkuu wa wilaya alisema maneno yaho katika ufunguzi wa mazoezi kisha akayaongoza kwakukimbia umbali wa Kilometa 6 kutoka ofisi za Halmashauri ya Wilaya Buhigwe.


Kanali Marco Gaguti (Mkuu wa wilaya ya Buhigwe) Kulia mwa picha. Akitowa meneno ya ufunguzi wa mazoezi hyo


Namkurugenzi wa Halmashauri pia alishiriki kikamilifu ili kuhamashisha nawengine kufanya mazoezi hayo.
Nd. Anost Nyamoga (Kushoto mwa picha) Mkurugenzi wa Halmashauri akiwa akipasha misuli moto kabla ya kuanza kukimbia mbio za Kilometa 6
 Michezo ilipatikana baada ya kukimbia umbali ya Kilometa 6, ni kama ifuatayo:-
i. Kukimbiza kuku kwa wafanya kazi wa Halmashauri pamoja na MDs
ii. Mbio za maguni
iii. Kupiga pushapu kwa MDs na kwa watumishi wenye uwezo wakufanya hivyo.

Mazoezi yote hayo yaliongozwa na kusimamiwa na Mkuu wa Wilaya Mwenye, Kama katika picha zinavyoonesha.

Yafuatayo ni matukio kwa njia ya picha kwa kila mazoezi.

Mkuu wa Wilaya Akiongoza MDs katika Mbio za Kilometa 6 Wakifuatiwa na Watumishi wa Halmashauri.

Nd. Bakena (DT wa Halmashauri Buhigwe) ni miongoni mwa washiriki wa mbio hizo.


Watumishi wa Halmashauri wakiwa katika ushiri wao wa mazoezi


Matembezi ya Kilometa 6 kwa watumishi

Mkuu wa Kitengo Cha Ugavi na Manunuzi (PMU) Kusho mwa picha  Nd. Magengele pamoja na Fundi umeme wa Halmashauri Bw. John Kaboto
Add caption

Pushapu kwa baadhi ya Md na Watumishi walioweza kufanya hivyo wakisimamiwa na Mkuu wa Wilaya.

Mkuu wa Wilaya akiwa anaongoza mazoezi hayo baada ya kumaliza mbio za kilometa 6

Mshindi wa mbio za Kuku. Akiwa ameshikilia zawadi yake.

Mbio za Magunia kwa Wanawake

Mbio za Maguni kwa wazee umri kati ya 50-55