Saturday 28 October 2017

Filled Under:

KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI LA KUFUNGA MWAKA


                           Kikao cha baraza la Madiwani kilianza kwa kamati kukutana kwaajili ya  kuvunja kamati hizo. Kwakuwa hiki ni kikao cha mwisho wa mwaka na kutokana na kanunu na sharia Kabla ya kuunda baraza jipya pamoja na kuteua Mwenyekiti Mwengine kwa mwaka wa fedha 2017/18 kamati hizo zinatakiwa zivunje ili kuteua kamati mpya pamoja na wenyeviti wake.
Kikao hiki kilikuwa na Agenda kuu zifuatazo.
1.      1.  Kufungua kikao.
2.      2.  Taarifa ya utekelezaji ya Mwaka 2016/17.
3.       3. Ratiba ya vikaa vya kisheria vya Halmashauri.
4.      4.  Uchaguzi wa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti.
5.       5. Mengineyo.
6.      6.  Kufunga kikao.

Baada ya kuwasilishwa kwa Agenda tajwa hapo juu, Makamu mwenyekiti Mh. Diwani Luzibila kutoka kata Munzeze alifungua kikao kwa kusoma Dua ya kikao hicho kwa kikiombea amani na Busara iwaongeza katika kufanya maamuzi kwaajili ya Halmashauri.
Makamu Mwenyekiti akifungua kikao kwa dua ya Pamoja.


Wagombea katika ngazi ya Mwenyekit wa Halmashauri.

Wagombea katika ngazi ya Makamu mwenyekti

 Baadaya ya uchaguzi matokeo ya kura yalikuwa kama ifuatavyo:-
UPANDE WA MWENYEKITI:
JUMLA YA KURA: 27
KURA ILIYOHARIBIKA: 1
Mh. VINANCE KIGWINYA: Alipata kura 16
Mh. MOSHI BUKEBUKE:  Alipata kura 10


UPANDE WA MAKAMU MWENYEKITI:
JUMLA YA KURA: 27
KURA ILIYOHARIBIKA: 1
Mh. HAMIS LUKANKA: Alipata kura 16
Mh. PASCAL NKEYEMBA:  Alipata kura 10

Baada ya matakeo hayo Mwenyekiti alimtanga Mh. Venance Kigwinya (Diwani wa kata ya Buhigwe) kuwa ni Mwenyekiti Mpya wa Halmashauri ya Wilaya Buhigwe.
Aidha kwa upande kwa Makamu Mwenyekiti, Mh. Hamis Lukanka ndio makamu mwenyekiti kwa Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe.

Waheshimiwa Makamu Mwenyekiti na Mwenyekiti wa Wilaya ya Buhigwe Baada ya kushinda uchaguzi.

0 comments:

Post a Comment