Tuesday 6 September 2016

Filled Under:

ZIARA YA MKUU WA MKOA MHE. BRG. (MST) EMMANUEL E. MAGANGA KATIKA WILAYA YA BUHIGWE.




ZIARA YA MKUU WA MKOA MHE. BRG. (MST) EMMANUEL E. MAGANGA KATIKA WILAYA YA BUHIGWE. tarehe 05-07/09/2016
 
MHE. BRG (MST) EMMANUEL MAGANGA aliwasili katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya mnamo saa 3:20 asubuhi na kusaini vitabu vya wegeni, pamoja na zoezi hilo liliendana na kutambulisha wakuu wa Idara pamoja na Waheshimiwa Madiwani. Baadaye alipokea taarifa fupi ya Halmashauri ya wilaya Buhigwe kupitia kwa Afisa Mipango.
 
Mkuu wa Mkoa Mhe. BRG Emmanuel E Maganga (Kushoto) akisalimiana na Mhe. Elisha K Bagwanya(M/kiti wa Halmashauri ya Wilaya Buhigwe)
Mhe Mkuu wa Mkoa Akisalimiana na Mkurugenzi Wa Halmashauri ya wilaya Buhigwe Nd. Anosta Nyamoga(Kulia mwa picha)

Ratiba iliendelea kwa kuanza kutembelea patakapo kuwa ofisi za makao makuu ya wilaya ya Buhigwe pamoja na kufanya ukaguzi wa majengo hiyo pamoja na nyumba za  wa watumishi wakuu, Mkuu wa Wilaya (DC), Katibu tawala (DAS) na badhi ya nyumba za waku wa Idara

 
Mkuu wa Wilaya Col. Marco Elisha Gaguti(Kulia mwa PIcha) akimtambulisha Mhe. BRG. GEN (MST) Emmanual Maganga Katika Makao Makuu ya Wilaya Buhigwe
 
Eng. Wa Halmashauri (wapili kulia mwa picha) akifafanua na Kumuelekeza Mhe Mkuu wa Mkoa Michoro ya jengo hilo


Afisa Mipango wa wilaya ND. Mduma akifafanua Mradi huo Wa Ofisi za Halmashauri ilipo fikia

Ukaguzi wa Jengo na Mkuu wa Mkoa Uliendelea







Hizi ni nyumba za Wakuu wa IDARA PAMOJA NA NYUMBA ZA DC pamoja Na DAS

Baada ya zoezi hilo Mkuu wa Mkoa alikutana na kuzungumza na Watumishi wa Halmashauri (HQ) pamoja na Waheshimiwa Madiwani.




M/Kiti wa Halmashauri (Mhe. Elisha K. Bagwanya) akitoa neno la Shukran kwa kutembelewa na Mkuu Mkuu Wa Mkoa

Mkuu wa Wilaya (Col. Marco Elisha Gaguti- aliyesimama ) akimkaribisha Mkuu wa Mkoa Kwaajili ya kuhutubia Wataalam pamoja na Waheshimiwa Madiwani

Mkuu wa Mkoa Akihutubia Waheshimiwa Madiwani pamoja na Wafanya Kazi wa Halmashauri


Katika kikao hicho mkuu wa Mkoa alitowa hutba fupi kwa watumishi pamoja na Waheshimiwa Madiwani.
Alisisitiza yafuatayo:
1.      Ukusanyaji wa mapoto kwa Halmashauri
Katika hili Mhe. BRG alisisitiza juu ya ukusanyaji wa mapato pamoja na kuboresha ukusanyi huo, huku akisisitiza juu ya 10% ya mgawanyo baada ya ukusanyaji huo wa mapato katika mchanganuo wa 5% kwa Vijana na 5% kwa Wanawake. Alimkumbusha Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri na Mkurugenzi mtendaji juu ya kutenga mgawanyo huo
2.      Utuzaji wa Amani katika Mkoa wetu
3.      Napia alisisitiza kwa Madiwani kuwa Milioni 50 za Mhe. Rais wa Awamu ya Tano Dr. John P Makufuli kuwa hizo pesa zipo na wananchi wajiandaa zinakuja
4.      Uhamiaji wa Haramu
Aliwakumbusha kuwa ukiumuhifadhi mhamiaji Haramu katika Mji wako (Kaya) basi ni kosa na inatakiwa ipigwe vitwa swala hili kwa nguvu zote.

Baada ya Makikao hicho Mkuu wa Mkoa alitembelea Wodi ya Wazazi kituo cha Afya cha Muyama.
Nakuzungumza na Wauguzi wa Wadi hiyo pamoja na Kuwatembelea Wazazi katika wodi hiyo.
Mradi huu wa kituo cha Afya cha Muyama ulidhaminiwa na  World Vision kwakuwajengea jengo hilo, na liliziduliwa Na Ndugu. George Jackson Mbijima Ambaye alikuwa kiongozi wa mbio za mwenge 18/07/2016 Katika siku ya Mwenge

Hospitali ya Mwayaya


Mkuu Wa Mkoa Akimpongeza Miongoni mwa Wazazi walio jifungua katika Hospitali hiyo

Baada ya hapo MHE. MKUU Wa Mkoa alitembelea  Kata ya Kajana katik Ujenzi wa Madarasa, Nyumba na Vyoo katika shule ya sekondari ya Nyamilambo. Alipongeza Mradi huu na kusisitiza Mkandarasi alipwe mapema ili mradi huu upate kuisha mapema iwezekanvyo.

 
Msafara wa Mkuu wa Mkoa

Mhandisi wa Wilaya pamoja Mkuu wa Mkoa

Afisa Elimu Sekondari akitoa taarifa fupi juu ya Shule ya Nyamilambo (Bi. Macelna Mbehom)




Moja ya Majengo ya Mradi huu wa shule


Alikwenda kutembelea Mradi wa ufugaji Samaki katika bwawa la Wanakijiji cha Mugera hasa kwa kikundi cha Wajasiliamali, kisha  alikutana na Wananchi wa Kijiji Mugera na kufanya Mkutano wake wa kwanza wa Hadhara katika Halmashauri ya wilaya ya Buhigwe.
Aliongea na Wananchi nakuwasisitiza yafuatayo:
i.                    Upimwajiwa Ardhi kwaajili ya mpango mijiya kiwilaya
ii.                  Ukusanyaji wa Kodi
iii.                Kuto kufumbia macho swala la Uhamiaji Haramu katika mkoa huu wa Kigoma

 
Afisa Uvuvi (Nd. James Kagaba) Akimuelezea Mkuu Wa Mkoa Mradi huu wa Ufugaji wa Masaki ulipofikia

Taarifa fupi Juu ya Mradi wa Wasaki

Mkuu wa Mkoa akipongeza Mradi wa Samaki kwa kuwazawadia kikundi hicho shiling 50,000/ kama pongezi kwao


Mkuu Wa Mkoa Akihutubia Wananchi katika kijiji cha Mugera




0 comments:

Post a Comment