![]() |
| Jengo la kituo cha afya kata ya Munzeze ambalo wananchi wamejitokeza kufyatua tofali kuendeleza ukamilishaji wa jengo hilo |
Tuesday, 18 July 2017
UZINDUZI WA BENKI YA MATOFALI KATA YA MUNZEZE
Sunday, 15 January 2017
UZINDUZI WA MAZOEZI KWA MATUMISHI WA UMMA KATIKA HALMASHAURI YA BUHIGWE
"Mazoezi ni afya"
Kupitia ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe mkoa Kigoma, siku ya Jumamosi (14.01.2017) ilizindua rasmi mazoezi kwa watumishi wa Halmashauri. "Lengo kuu ya mazoezi hayo nijenga mwili na kujiepusha na magonjwa yasio ambukiza, kama vile ugonjwa wa presha ya damu, kuongezeka uzito niongoni mwatatizo kubwa kwa wengi mwa watumishi wa umma, kupitia mazoezi hayo ambayo yanataraji kufanyika kila jumamosi ya wiki ya pili ya mwezi"
Mkuu wa wilaya akataja faida zipatikanazo kwa kufanya mazoezi.
1. Mazoezi ya mwili husaidia kulirekebisha shinikizo la Damu.
2. Mazoezi ya Mwili huiruhusu damu nyingi zaidi kuzifikia sehemu zote za mwili na kuifanya mikono na miguu ipate joto.
3. Mazoezi ya mwili yanaondoa mambo yote ya mwili, yaani mkazo wa mwili na mfashaiko wa moyo na kukusaidia wewe kujisikia vizuri zaidi katika maisha yako. Mazoezi ni tiba bora.
4. Mazoezi ya mwili hujenga afya yako
5. Mazoezi ya mwili huimarisha misuli pia nakunawirisha mwili kwa ujumla
6. Mazoezi huongeza ufanisi makazini
Mkuu wa wilaya alisema maneno yaho katika ufunguzi wa mazoezi kisha akayaongoza kwakukimbia umbali wa Kilometa 6 kutoka ofisi za Halmashauri ya Wilaya Buhigwe.
![]() |
|
Kanali Marco Gaguti (Mkuu wa wilaya ya Buhigwe) Kulia mwa picha. Akitowa meneno ya ufunguzi wa mazoezi hyo
|
Namkurugenzi wa Halmashauri pia alishiriki kikamilifu ili kuhamashisha nawengine kufanya mazoezi hayo.
![]() |
| Nd. Anost Nyamoga (Kushoto mwa picha) Mkurugenzi wa Halmashauri akiwa akipasha misuli moto kabla ya kuanza kukimbia mbio za Kilometa 6 |
i. Kukimbiza kuku kwa wafanya kazi wa Halmashauri pamoja na MDs
ii. Mbio za maguni
iii. Kupiga pushapu kwa MDs na kwa watumishi wenye uwezo wakufanya hivyo.
Mazoezi yote hayo yaliongozwa na kusimamiwa na Mkuu wa Wilaya Mwenye, Kama katika picha zinavyoonesha.
Yafuatayo ni matukio kwa njia ya picha kwa kila mazoezi.
![]() |
| Mkuu wa Wilaya Akiongoza MDs katika Mbio za Kilometa 6 Wakifuatiwa na Watumishi wa Halmashauri. |
![]() |
| Nd. Bakena (DT wa Halmashauri Buhigwe) ni miongoni mwa washiriki wa mbio hizo. |
![]() |
| Watumishi wa Halmashauri wakiwa katika ushiri wao wa mazoezi |
![]() |
| Matembezi ya Kilometa 6 kwa watumishi |
![]() |
| Mkuu wa Kitengo Cha Ugavi na Manunuzi (PMU) Kusho mwa picha Nd. Magengele pamoja na Fundi umeme wa Halmashauri Bw. John Kaboto |
![]() |
| Add caption |
![]() |
| Pushapu kwa baadhi ya Md na Watumishi walioweza kufanya hivyo wakisimamiwa na Mkuu wa Wilaya. |
![]() |
| Mkuu wa Wilaya akiwa anaongoza mazoezi hayo baada ya kumaliza mbio za kilometa 6 |
![]() |
| Mshindi wa mbio za Kuku. Akiwa ameshikilia zawadi yake. |
![]() |
| Mbio za Magunia kwa Wanawake |
![]() |
| Mbio za Maguni kwa wazee umri kati ya 50-55 |
![]() |
Wednesday, 19 October 2016
KIKAO CHA KWANZA CHA BARAZA LA BIASHARA BUHIGWE
Kwa awamu ya kwanza, Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe ilifanikiwa kufanya kikao cha kwanza cha baraza la biashara Octoba 18, 2016 kilichodhaminiwa na Local Goverment Climate (LiC)
Kikao hicho kilichofanyika Wilayani hapa na kuhudhuriwa na mwenyekiti wake Kanali Marco Gaguti (Mkuu wa wilaya ya Buhigwe), akiambatana na katibu wa baraza hilo (Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Buhigwe Ndg Sadock Kihuriko), pamoja na wawakilishi wa LiC mkoa wa Kigoma, wawakilishi kutoka sekta mbalimbali na wajumbe wa baraza hilo.
Kikao hicho kilijadili agenda kuu nne
- Elimu ya biashara na ujasiliamali (Business and entrepreneurship Training).
- uwezekano wa kuboresha/mikakati ya kusaidia uwekezaji (access to finance/investment support stratergies).
- mikakati ya mwelekeo wa vipaumbele vya minyororo ya thamani (Stratergic direction for priority).
Mwenyekiti wa kikao cha baraza la biashara (Kanali Marco Gaguti) akifungua rasmi kikao hicho na kutoa maelezo na umuhimu wa baraza hilo hasa katika kuonesha fursa, changamoto na hata mikakati ya nini kifanyike ili kunufaika na uwepo wa baraza hilo katika kuleta manufaa ya wanabuhigwe kwa ujumla na kuboresha mapato ya Halmashauri kwa kupitia fursa za biashara.
"Mazingira Bora ya biashara kwa kukuza mapato ya ndani ya Halmashauri"
| Baadhi ya wajumbe wa baraza kutoka sekta tofauti wakisikiliza agenda ya mikopo kutoka mwakilishi wa NMB Kasulu |
Agenda ya Mikakati ya mwelekeo wa vipaumbele vya minyororo ya thamani, ilijadiliwa. katika agenda hii suala la upatikanaji wa pembejeo za kilimo, kutokuwepo kwa viwanda kwa ajili ya usindikaji wa mazao yaliyo uti wa mgongo wilayani yalidaliwa na zaidi ya yote uboreshwaji wa mnada wa wilaya na majosho.
| Ndg Boniface Nanda (Afisa kilimo wilaya) akifafanua suala la pembejeo na uwepo wa viwanda vya usindikaji mazo yapatikanayo katika wilaya yetu na hata namna ya kupata mitambo ya kufanyia kazi hiyo. |
|
Katika kikao hicho, wajumbe na wadau waliguswa na agenda zilizoandaliwa na mafisa biashara wa wilaya na hivyo kuwafanya washiriki vilivyo katika kikao.
| Ndg Philemon Home ( mdau kutoka taasisi binafsi) akichangia agenda ya kilimo, hasa katika upatikanaji wa pembejeo na mifugo katika majosho na mnada |
Katika suala la kilimo ambamo jamii kubwa inajihusisha kwa ujumla, suala la upatikana wa pembejeo kwa bei nafuu na hata kupata mitambo/mashine za usindikaji wa baadhi ya mazao yalimwayo wilayani hapa, mdau Ayubu Fidel (sekta binafsi) hakusita kuzungumzia umuhimu na uhitaji wa vitu hivyo kwa wakulima wa wilaya ya Buhigwe mbele ya mwenyekiti Kanali Marco Gaguti na balaza lake kwa ujumla.
| Ndg Ayubu Fidel Chanko (Mdau sekta binafsi) |
Suala la ukamilishwaji wa ujenzi wa kituo cha biashara (one stop business centre) nalo halikuachwa kama mengineyo katika kikao hicho na aliyewakilisha sekta binafsi wilaya ya Buhigwe Ndg Venance Kigwinya, akashauri baraza kwa kupitia usimamizi wa mwenyekiti wake kukamilisha utafiti na hata ujenzi wa kituo hicho ifikapo Januari 2017 kama ilivyoahidiwa na meneja wa LiC mkoa wa Kigoma Dr Betty Mlingi.
| Ndg Venance Kigwinya, akifafanua juu ya umuhimu wa kituo hicho cha biashara kilivyo na tija kwa wafanya biashara wa wilaya ya Buhigwe |
Kwa mamlaka aliyonayo, mwenyekiti wa baraza kabla ya kufunga kikao alitoa nafasi kwa wageni toka nje ya wilaya ya Buhigwe kutoa japo neno kuhusu mjadala wa agenda za siku hiyo na ndipo Ndg Francis Peter (kutoka LiC Dodoma) akatoa hongera zake kwa mwenyekiti (Mkuu wa wilaya ya Buhigwe) Kanali Marco Gaguti kwa kuwa na timu nzuri iliyoonesha uchu na nia ya kuyatekeleza yote yaliyojadiliwa ili kutoa matunda bora kwa jamii. Mwakilishi huyo hakusita kupongeza namna agenda zilivyoandaliwa na zaidi ya yote kujali muda zaidi katika kujadili hoja hizo
| Ndg Francis Peter (Akiwakilisha LiC Dodoma) |
Akihitimisha na kufanga kikao mwenyekiti wa baraza la biashara la wilaya ya Buhigwe Kanali Marco Gaguti alitoa shukrani zake kwa wageni kutoka LiC na hata wale walioalikwa kutoka sekta tofautitofauti na zaidi yayote wajumbe wa baraza hilo na kufunga kikao hicho rasmi.
| Mwenyekiti wa baraza la biashara la wilaya ya Buhigwe Kanali Marco Gaguti akifunga kikao cha kwanza cha baraza la biashara wilaya ya Buhigwe |
Mwenyekiti wa baraza la biashara akiwa katika picha ya pamoja na wageni na wajumbe wa baraza zima la biashara la wilaya ya Buhigwe.
Monday, 26 September 2016
WAZIRI WA NISHATI NA MADINI AFANYA ZIARA KATIKA WILAYA WA BUHIGWE KUKAGUA MIRADI YA UMEME NA KUZUNGUMZA NA WANANCHI
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akipokelewa na baadhi ya watendaji kutoka katika Halmashauri ya wilaya buhigwe pamoja na wafanyakazi wa Shirika la Umeme Nchini (Tanesco) mara baada ya kuwasili katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya Buhigwe.
Ziara hii ilikuwa ya siku moja na kutembelea vijiji vitatu:-
Mradi wa REA 2 ulitengemea kukamilika tarehe 30/09/2016 lakini kutokana na idadi ndogo ya maombi ya umeme Mh. Waziri aliagiza kusogeza muda kwa mwezi mmoja ili kupata kutoa fursa kwa wengine kujiandikisha katika na kufanya maombi kwaajili ya kupa huduma hiyo. Kwahiyo Mradi huu utafikia kikomo mnamo tarehe 30/10/2016.
Pia alimuagiza Msimamizi wa Mradi wa REA pamoja na Meneje tanesco kwaajili ya kutoa mafunzo juu kifaa kipya kijulikanacho kwajina la Umeme tayari. Kifaa hili kinafanya kazi sawa na swichi kuu ya Umeme "Main Switch".
Faida ya kifaa hiki ni kupunguza gharama ya umeme katika kufunga wayaringi katika nyumba ya mteja.
![]() |
Ziara hii ilikuwa ya siku moja na kutembelea vijiji vitatu:-
- Kijiji cha Kasumo
- Kijiji cha Buhigwe
- kijiji cha Manyovu (Munanila)
Mradi wa REA 2 ulitengemea kukamilika tarehe 30/09/2016 lakini kutokana na idadi ndogo ya maombi ya umeme Mh. Waziri aliagiza kusogeza muda kwa mwezi mmoja ili kupata kutoa fursa kwa wengine kujiandikisha katika na kufanya maombi kwaajili ya kupa huduma hiyo. Kwahiyo Mradi huu utafikia kikomo mnamo tarehe 30/10/2016.
Pia alimuagiza Msimamizi wa Mradi wa REA pamoja na Meneje tanesco kwaajili ya kutoa mafunzo juu kifaa kipya kijulikanacho kwajina la Umeme tayari. Kifaa hili kinafanya kazi sawa na swichi kuu ya Umeme "Main Switch".
Faida ya kifaa hiki ni kupunguza gharama ya umeme katika kufunga wayaringi katika nyumba ya mteja.
![]() |
| Kifaa cha Umeme Tayari |
Thursday, 8 September 2016
SIKU YA PILI YA ZIARA YA MKUU WA MKOA
Siku ya pili
ya ziara ilikuwa nikwenda kuzindua benki ya
matofali katika kijiji cha Kibwigwa. Benki hiyo ilikuwa na jumla ya
matofali 150,000 . Matofali hayo
yatatumika katika kujenga baadhi ya matundu ya vyoo.
| Mkuu wa Mkoa akizindua Uchomaji wa Benki hiyo ya Matofali katika kijiji cha Kibwigwa |
Pia Mkuu
wa Mkoa alizindua rasmi Nyumba kumi za kiusalama kwa lengo la kuboresha usalama
wa Wilaya na Mkoa kiujumla katika mipaka yote inayozunguka. Nyumba kumi hizo
zilizo zinduliwa katika kata ya Munanila.
| Mmoja wa kaya Lengwa akiwa ametembelewa na Mhe. Mkuu wa Mkoa |
| Mmoja wa Wajumbe wa Nyumba 10 za kiusalama B. Diseli Chupa (Wakwanza Kulia) |
Subscribe to:
Posts (Atom)

























