Tuesday, 18 July 2017

UZINDUZI WA BENKI YA MATOFALI KATA YA MUNZEZE

UZINDUZI WA BENKI YA MATOFALI KWA AJILI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA KATA YA MUNZEZE WILAYA YA BUHIGWE.
Halmashauri ya wilaya ya Buhigwe imezindua benki ya matofali kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya kata ya Munzeze. uzinduzi huo umefanyika julai 14, 2017 na kuhudhuriwa na afisa tawala wa wilaya Bw Peter Masindi (kwa niaba ya mkuu wa wilaya ya Bhigwe), mkurugenzi mtendaji wa halmashauri Bw Anosta Nyamoga, OCD wa wilaya Bw Venance Mapala na mwenyeji wao mheshimiwa Wilson Luzibira (Diwani wa kata hiyo).
Uzinduzi huo ambao ulikadiriwa kuwa na lengo la kufyatua tofali elfu kumi (10,000) kwa ajili ya umaliziaji wa kituo hicho cha afya. Viongozi hao wa wilaya wamliwasihi wananchi waendelee na moyo wa kujitowa kuleta maendeleo yao wenyewe na kuwakumbusha kuwa serikali ipo nao kukamilisha juhudi zao hizo. Zaidi ya hayo, viongozi hao wa wilaya walitoa rai kwa wananchi wa wilaya hiyo kuiga mfano wa kuigwa wa wananchi wa kata ya Munzeze kwa kile walichokifanya siku hiyo.

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Buhigwe Bw Anosta Nyamoga akishirikiana na wananchi wa kata ya Munzeze kuandaa udongo kwa ajili ya kufyatua tofali kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya kata ya Munzeze


Wananchi wa kata ya Munzeze wilayani Buhigwe wakionesha ari yao katika siku ya uzinduzi wa benki ya matofali kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya katika kata yao.

Baadhi ya wanakamati ya ulinzi na usalama, akishiriki kwenye zoezi zima la ufyatuaji wa matofali katika siku ya uzinduzi wa benki ya matofali kata ya Munzeze

Jengo la kituo cha afya kata ya Munzeze ambalo wananchi wamejitokeza kufyatua tofali kuendeleza ukamilishaji wa jengo hilo







Sunday, 15 January 2017

UZINDUZI WA MAZOEZI KWA MATUMISHI WA UMMA KATIKA HALMASHAURI YA BUHIGWE



"Mazoezi ni afya"
 Kupitia ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe mkoa Kigoma, siku ya Jumamosi (14.01.2017) ilizindua rasmi mazoezi kwa watumishi wa Halmashauri. "Lengo kuu ya mazoezi hayo nijenga mwili na kujiepusha na magonjwa yasio ambukiza, kama vile ugonjwa wa presha ya damu, kuongezeka uzito niongoni mwatatizo kubwa kwa wengi mwa watumishi wa umma, kupitia mazoezi hayo ambayo yanataraji kufanyika kila jumamosi ya wiki ya pili ya mwezi"

Mkuu wa wilaya akataja faida zipatikanazo kwa kufanya mazoezi.
1. Mazoezi ya mwili husaidia kulirekebisha shinikizo la Damu.
2.  Mazoezi ya Mwili huiruhusu damu nyingi zaidi kuzifikia sehemu zote za mwili na kuifanya mikono na miguu ipate joto.
3. Mazoezi ya mwili yanaondoa mambo yote ya mwili, yaani mkazo wa mwili na mfashaiko wa moyo na kukusaidia wewe kujisikia vizuri zaidi katika maisha yako. Mazoezi ni tiba bora.
4. Mazoezi ya mwili hujenga afya yako
5. Mazoezi ya mwili huimarisha misuli pia nakunawirisha mwili kwa ujumla
6. Mazoezi huongeza ufanisi makazini

Mkuu wa wilaya alisema maneno yaho katika ufunguzi wa mazoezi kisha akayaongoza kwakukimbia umbali wa Kilometa 6 kutoka ofisi za Halmashauri ya Wilaya Buhigwe.


Kanali Marco Gaguti (Mkuu wa wilaya ya Buhigwe) Kulia mwa picha. Akitowa meneno ya ufunguzi wa mazoezi hyo


Namkurugenzi wa Halmashauri pia alishiriki kikamilifu ili kuhamashisha nawengine kufanya mazoezi hayo.
Nd. Anost Nyamoga (Kushoto mwa picha) Mkurugenzi wa Halmashauri akiwa akipasha misuli moto kabla ya kuanza kukimbia mbio za Kilometa 6
 Michezo ilipatikana baada ya kukimbia umbali ya Kilometa 6, ni kama ifuatayo:-
i. Kukimbiza kuku kwa wafanya kazi wa Halmashauri pamoja na MDs
ii. Mbio za maguni
iii. Kupiga pushapu kwa MDs na kwa watumishi wenye uwezo wakufanya hivyo.

Mazoezi yote hayo yaliongozwa na kusimamiwa na Mkuu wa Wilaya Mwenye, Kama katika picha zinavyoonesha.

Yafuatayo ni matukio kwa njia ya picha kwa kila mazoezi.

Mkuu wa Wilaya Akiongoza MDs katika Mbio za Kilometa 6 Wakifuatiwa na Watumishi wa Halmashauri.

Nd. Bakena (DT wa Halmashauri Buhigwe) ni miongoni mwa washiriki wa mbio hizo.


Watumishi wa Halmashauri wakiwa katika ushiri wao wa mazoezi


Matembezi ya Kilometa 6 kwa watumishi

Mkuu wa Kitengo Cha Ugavi na Manunuzi (PMU) Kusho mwa picha  Nd. Magengele pamoja na Fundi umeme wa Halmashauri Bw. John Kaboto
Add caption

Pushapu kwa baadhi ya Md na Watumishi walioweza kufanya hivyo wakisimamiwa na Mkuu wa Wilaya.

Mkuu wa Wilaya akiwa anaongoza mazoezi hayo baada ya kumaliza mbio za kilometa 6

Mshindi wa mbio za Kuku. Akiwa ameshikilia zawadi yake.

Mbio za Magunia kwa Wanawake

Mbio za Maguni kwa wazee umri kati ya 50-55




Wednesday, 19 October 2016

KIKAO CHA KWANZA CHA BARAZA LA BIASHARA BUHIGWE

           
Kwa awamu ya kwanza, Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe ilifanikiwa kufanya kikao cha kwanza cha baraza la biashara Octoba 18, 2016 kilichodhaminiwa na Local Goverment Climate (LiC)
             Kikao hicho kilichofanyika Wilayani hapa na kuhudhuriwa na mwenyekiti wake Kanali Marco Gaguti (Mkuu wa wilaya ya Buhigwe), akiambatana na katibu wa baraza hilo (Kaimu Mkurugenzi wa  Halmashauri ya Buhigwe Ndg Sadock Kihuriko), pamoja na wawakilishi wa LiC mkoa wa Kigoma, wawakilishi kutoka sekta mbalimbali na wajumbe wa baraza hilo.
             Kikao hicho kilijadili agenda kuu nne

  1. Elimu ya biashara na ujasiliamali (Business and entrepreneurship Training).
  2. uwezekano wa kuboresha/mikakati ya kusaidia uwekezaji (access to finance/investment support stratergies).
  3. mikakati ya mwelekeo wa vipaumbele vya minyororo ya thamani (Stratergic direction for priority).
Mwenyekiti wa kikao cha baraza la biashara (Kanali Marco Gaguti) akifungua rasmi kikao hicho na kutoa maelezo na umuhimu wa baraza hilo hasa katika kuonesha fursa, changamoto na hata mikakati ya nini kifanyike ili kunufaika na uwepo wa baraza hilo katika kuleta manufaa ya wanabuhigwe kwa ujumla na kuboresha mapato ya Halmashauri kwa kupitia fursa za biashara.
"Mazingira Bora ya biashara kwa kukuza mapato ya ndani ya  Halmashauri"
Katikati ni mwenyekiti wa baraza Kanali Marco Gaguti, kulia kwake  Katibu wa baraza la biashara Kaimu mkurugenzi Ndg Sadock Kihuriko na kushoto kwake mwenyekiti wa TCCIA wilaya ya Buhigwe Ndg Azaria Kalobho.

Baada ya ufunguzi wa Mwenyekiti wa Baraza hilo, akatoa  fursa kwa wajumbe wa baraza hilo kuanza kujadili agenda za kikao hicho. Katika kujadili agenda za kikao, Mwenyekiti aliomba wajumbe na wawakilishi kutoka sekta binafsi kutoa japo historia ya soko la Nyamugali angalau kwa wajumbe kujuwa umuhimu wa soko hilo katika kumnufaisha mwanainchi mfanyabiashara na hata Halmashauri katika kuongeza mapato yake. 
Bwana Paul Bahinda  mwakilishi kutoka Buhigwe Green Innovation (BGI), akitoa historia ya soko hilo na faida zake kwa watumiaji na nini kifanyike katika kuboresha soko ili lengo la kumnufaisha mfanyabiashara litimie na hata mapato ya Halmashauri pia. (Picha hapo chini)




Katika mjadala huu ilibidi meneja wa LiC mkoa wa Kigoma Dr Betty Mlingi (Pichani chini) kutoa ufafanuzi wa namna LiC inavyojitokeza kusaidia baadhi ya miradi ambayo inakuwa imeshafanyiwa tathmini na ufuatiliaji wa karibu wa mradi husika. Na baada ya hapo ndipo LiC yajitokeza kuunga mkono kufanisha mradi huo.


Katika agenda hiyo, mwenyekiti alishauri azimio litolewe na andiko liandikwe na kazi ya soko hilo ifanyike. Zaidi ya yote mwenyekiti wa baraza Kanali Marco Gaguti (pichani chini) alitia nia ya kuchukua dhamira kulifanikisha hilo akishirikiana na mkurugenzi wa Halmashauri na wadau kutoka sekta mbalimbali ya kitu gani kifanyike.



Agenda ziliendelea kujadiliwa na hapa ndipo suala la kukopesheka likajadiliwa kama moja ya agenda kikaoni.
Katibu wa baraza, Ndg Saddock Kihuriko (Kaimu mkurugenzi wa wilaya katika baraza) akikaribisha agenda ya uwezekano wa kukopesheka.

Agenda hii ilibeba na hoja ya kutopatikana kwa benki katika wilaya na hivyo kufanya wafanyabiashara kupata taabu ya namna ya ubebaji wa fedha zao hasa wakati wa kwenda kwenye magulio na hata kuhatarisha maisha yao.
Akielezea suala hilo kikaoni, afisa mikopo wa benki ya NMB Kasulu, Bw. Kulwa Shotto (Pichani chini) alilihakikishia baraza kuwa benki hiyo imepata nafasi wilayani kwa ajili ya kujenga tawi dogo na kuanza kutoa huduma hiyo ifikapo mwezi wa Disemba mwaka huu.
Zaidi ya yote, afisa mikopo huyo aliwaondoa wasiwasi wana baraza hilo kwa niaba ya wajasiliamali wengine kuwa NMB wapo kuwakopesha wafanyabiashara kwa ajili ya kufanikisha malengo yao kibiashara.




Baadhi ya wajumbe wa baraza kutoka sekta tofauti wakisikiliza agenda ya mikopo kutoka mwakilishi wa NMB Kasulu


Agenda ya Mikakati ya mwelekeo wa vipaumbele vya minyororo ya thamani, ilijadiliwa. katika agenda hii suala la upatikanaji wa pembejeo za kilimo, kutokuwepo kwa viwanda kwa ajili ya usindikaji wa mazao yaliyo uti wa mgongo wilayani yalidaliwa na zaidi ya yote uboreshwaji wa mnada wa wilaya na majosho.

Ndg Boniface Nanda (Afisa kilimo wilaya) akifafanua suala la pembejeo na uwepo wa viwanda vya usindikaji mazo yapatikanayo katika wilaya yetu na hata namna ya kupata mitambo ya kufanyia kazi hiyo.

Ndg Keneth Tefurukwa (Afisa mifugo wilaya) akitoa ufafauzi kwa baraza juu ya suala la uboreshwaji wa mnada wa wilaya na majosho.


Katika kikao hicho, wajumbe na wadau waliguswa na agenda zilizoandaliwa na mafisa biashara wa wilaya na hivyo kuwafanya washiriki vilivyo katika kikao.
Ndg Philemon Home ( mdau kutoka taasisi binafsi) akichangia agenda ya kilimo, hasa katika upatikanaji wa pembejeo na mifugo katika majosho na mnada  

Katika suala la kilimo ambamo jamii kubwa inajihusisha kwa ujumla, suala la upatikana wa pembejeo kwa bei nafuu na hata kupata mitambo/mashine za usindikaji wa baadhi ya mazao yalimwayo wilayani hapa, mdau Ayubu Fidel (sekta binafsi) hakusita kuzungumzia umuhimu na uhitaji wa vitu hivyo kwa wakulima wa wilaya ya Buhigwe mbele ya mwenyekiti Kanali Marco Gaguti na balaza lake kwa ujumla.

Ndg Ayubu Fidel Chanko (Mdau sekta binafsi)


Suala la ukamilishwaji wa ujenzi wa kituo cha biashara (one stop business centre) nalo halikuachwa kama mengineyo katika kikao hicho na aliyewakilisha sekta binafsi wilaya ya Buhigwe Ndg Venance Kigwinya, akashauri baraza kwa kupitia usimamizi wa mwenyekiti wake kukamilisha utafiti na hata ujenzi wa kituo hicho ifikapo Januari 2017 kama ilivyoahidiwa na meneja wa LiC mkoa wa Kigoma Dr Betty Mlingi.

Ndg Venance Kigwinya, akifafanua juu ya umuhimu wa kituo hicho cha biashara kilivyo na tija kwa wafanya biashara wa wilaya ya Buhigwe

Kwa mamlaka aliyonayo, mwenyekiti wa baraza kabla ya kufunga kikao alitoa nafasi kwa wageni toka nje ya wilaya ya Buhigwe kutoa japo neno kuhusu mjadala wa agenda za siku hiyo na ndipo Ndg Francis Peter (kutoka LiC Dodoma) akatoa hongera zake kwa mwenyekiti (Mkuu wa wilaya ya Buhigwe) Kanali Marco Gaguti kwa kuwa na timu nzuri iliyoonesha uchu na nia ya kuyatekeleza yote yaliyojadiliwa ili kutoa matunda bora kwa jamii. Mwakilishi huyo hakusita kupongeza namna agenda zilivyoandaliwa na zaidi ya yote kujali muda zaidi katika kujadili hoja hizo

Ndg Francis Peter (Akiwakilisha LiC Dodoma)


Akihitimisha na kufanga kikao mwenyekiti wa baraza la biashara la wilaya ya Buhigwe Kanali Marco Gaguti alitoa shukrani zake kwa wageni kutoka LiC na hata wale walioalikwa kutoka sekta tofautitofauti na zaidi yayote wajumbe wa baraza hilo na kufunga kikao hicho rasmi.



Mwenyekiti wa baraza la biashara la wilaya ya Buhigwe Kanali Marco Gaguti akifunga kikao cha kwanza cha baraza la biashara wilaya ya Buhigwe



Mwenyekiti wa baraza la biashara akiwa katika picha ya pamoja na wageni na wajumbe wa baraza zima la biashara la wilaya ya Buhigwe.

Mwenyekiti Kanali Marco Gaguti (katikati walioketi ), kutoka kushoto kwake ni meneja wa LiC mkoa wa Kigoma Dr Betty Mlingi mwenyekiti wa TCCIA wilaya ya Buhigwe Ndg Azaria Kalobho kulia kwake  Katibu wa baraza la biashara Kaimu mkurugenzi Ndg Sadock Kihuriko na Katibu tawala wilaya ya Buhigwe Ndg Peter Masindi,  

Monday, 26 September 2016

WAZIRI WA NISHATI NA MADINI AFANYA ZIARA KATIKA WILAYA WA BUHIGWE KUKAGUA MIRADI YA UMEME NA KUZUNGUMZA NA WANANCHI

Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akipokelewa na baadhi ya watendaji kutoka katika Halmashauri ya wilaya buhigwe pamoja na wafanyakazi wa Shirika la Umeme Nchini (Tanesco)  mara baada ya kuwasili katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya Buhigwe.






 

Ziara hii ilikuwa ya siku moja na kutembelea vijiji vitatu:-
  •  Kijiji cha Kasumo
  • Kijiji cha Buhigwe
  • kijiji cha Manyovu (Munanila)  
Nakatika vijiji vyote alikutuna na kuzungumza na wananchi ili kupata kero zao juu ya Mradi huu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA 2).





Mradi wa REA 2 ulitengemea kukamilika tarehe 30/09/2016 lakini kutokana na idadi ndogo ya maombi ya umeme Mh. Waziri aliagiza kusogeza muda kwa mwezi mmoja ili kupata kutoa fursa kwa wengine kujiandikisha katika na kufanya maombi kwaajili ya kupa huduma hiyo. Kwahiyo Mradi huu utafikia kikomo mnamo tarehe 30/10/2016.






 Pia alimuagiza Msimamizi wa Mradi wa REA pamoja na Meneje tanesco kwaajili ya kutoa mafunzo juu kifaa kipya kijulikanacho kwajina la Umeme tayari. Kifaa hili kinafanya kazi sawa na swichi kuu ya Umeme "Main Switch".

Faida ya kifaa hiki ni kupunguza gharama ya umeme katika kufunga wayaringi katika nyumba ya mteja.
Kifaa cha Umeme Tayari


 






 

Thursday, 8 September 2016

SIKU YA PILI YA ZIARA YA MKUU WA MKOA



Siku ya pili ya ziara ilikuwa nikwenda kuzindua benki ya  matofali katika kijiji cha Kibwigwa. Benki hiyo ilikuwa na jumla ya matofali  150,000 . Matofali hayo yatatumika katika kujenga baadhi ya matundu ya vyoo.
 
Moja ya Matanuri yapo tayari kwaajili ya kuchomwa


Mkuu wa Mkoa akizindua Uchomaji wa Benki hiyo  ya Matofali katika kijiji cha Kibwigwa



Pia Mkuu wa Mkoa alizindua rasmi Nyumba kumi za kiusalama kwa lengo la kuboresha usalama wa Wilaya na Mkoa kiujumla katika mipaka yote inayozunguka. Nyumba kumi hizo zilizo zinduliwa katika kata ya Munanila.


Mmoja wa kaya Lengwa akiwa ametembelewa na Mhe. Mkuu wa Mkoa

Mmoja wa Wajumbe wa Nyumba  10 za kiusalama B. Diseli Chupa (Wakwanza Kulia)